Kili Music Tour 2014 yakamilishwa kwa kishindo Dar

Kili Music Tour 2014 yakamilishwa kwa kishindo Dar

Tamasha la Kili Music Tour 2014 lilifungwa kwa staili ya aina yake katika viwanja vya Leaders Club ambapo wasanii wanaofanya vizuri nchini walilishambulia jukwaa kwa masaa nane mfululizo na kuzikonga nyoyo za maelfu waliojitokeza. Burudani usiku huo ilipambwa na Mashujaa Band, Mapacha Watatu, Malaika Band, Rich Mavoko, Vanessa Mdee, Jambo Squad, Ommy Dimpoz, Ben Pol, Khadija Kopa, Profesa Jay, Mwana FA, AY na Weusi.

Mvua iliyomwagika wakati fulani haikuwa kikwazo kwa mashabiki kuendelea kufurahia burudani na hadi mwisho wengi kuondoka wakiwa wameridhika.

2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 14 15 16 17 18 19 20 21 22.1 22 23 24 25 262525fsds25

Comments